Katika kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania, Kampuni ya Future Century Ltd, wakishirikiana na Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, inakuletea pambano la historia hapa nchini kwa kuwakutanisha wakongwe wa soka barani Afrika hao sio wengine ni Simba Sports Club (Wekundu wa Msimbazi) na Asante Kotoko ya Ghana, haijawahi kutokea.
Mtanange huu utafanyika tarehe 11-Desemba, 2011 katika uwanja wa Taifa na sio shamba la bibi saa kumi jioni.
Viingilio ni poa kabisa yaani TSh 30,000/= VIP A, 20,000/= VIP B, na 10,000/ VIP C wakati viti vya rangi ya Chungwa vitakuwa ni TSh 7,000/=, viti vya Blue vitakuwa TSh 5,000/= na kama haitoshi patakuwa na tiketi za TSh 3,000/= tu kwa viti vya Kijani.
Wahi tiketi yako mapema katika vituo vyote vya Big Bon, Oil Com, Zizou Fashion na Steers, hali kadhalika utapata tiketi zako toka Clouds FM, Vanne Fashions Tabata, VETA Chang'ombe, Mwembe Yanga, shule ya Benjamini Mkapa, Uwanja wa Taifa na Robby Fashion Kinondoni.
Pambano hili la kihistoria barani Afrika linaletwa kwenu na Future Century Ltd na PPF.
Usiwe muoga wa matukio makubwa. Njoo uwe mmoja wa marafiki wa Uhuru na kutengeneza historia kubwa ya soka ambayo haijawahi kutokea barani Afrika.
No comments:
Post a Comment