Saturday, December 10, 2011

Dondoo

ASANTE KOTOKO WAINGIA DAR
Asante Kotoko wakiwasili jiji Dar es Salaam

   Timu ya Asante Kotoko toka Ghana imeingia Dar es Salaam kupambana na timu ya Simba katika pambano la miaka 50 ya Uhuru, kesho uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
   Wakati huo huo leo ktakuwa na pambano kali kati ya Kilimanjaro Stars na Sudan kuwania nafasi ya tatu kombe la CECAFA, ikifuatiwa na fainali ya aina yake kati ya Rwanda na Uganda.
   Mapambano yote yatafanyika katika uwanja wa Taifa leo kuanzia saa 8:00 mchana.


KOMBE LA MAPINDUZI NETIBOLI

   Timu za netiboli kutoka Zambia na Zimbabwe zimethibisha kushiriki Kombe la Mapinduzi, pia timu kutoka Kenya na Uganda zimeshatumiwa mwaliko.
   Rahma Bakari, Katibu Mkuu wa (CHANETA) alisema tayari timu hizo zimethibitisha kushiriki na mashindano yanatarajiwa kuanza Januari mwakani.
   Mashindano hayo yanatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi milioni 100.


TUHUMA ZA MAKOCHA CECAFA ZATUPILIWA MBALI

   Tuhuma zilizopelekwa CECAFA na makocha mbalimbali wa timu shiriki zimetupiliwa mbali na uongozi, tuhuma hizo zimeelekezwa kwa marefa ya kwamba wanaonyesha upendeleo wa wazi kwa baadhi ya timu.
   Akizungumzia tuhuma hizo, Katibu Mkuu wa CECAFA bw. Nicholas Musonye aemesema tuhuma hizo si za kweli na marefa wote walichezesha sawa kwa kuzingatia sheria za FIFA.  

No comments:

Post a Comment

Post a Comment