Tuesday, December 13, 2011

Dondoo

KOSA GOLI YA MWAKA

Ama kweli duniani kuna mambo, mshambuliaji Oscar Cardozo wa Benfica amejizolea sifa za kukosa goli bora la mwaka, hebu jionee hii video fupi uwe shahidi.










MICHUANO YA KIKAPU TAIFA YATIMUA VUMBI
Mashindano ya Kikapu yaliyoanza juzi, yanaendelea kwa kasi ambapo jana timu ya Shinyanga Wanaume iliifunga Pemba Wanaume vikapu 82-46.Pemba Wanawake ilifanya kweli kuifunga Kilimanjaro Wanawake kwa vikapu 118-7, Mbeya imeicharanga Mara 62-49 upande wa wanawake. Singida Wanaume Imeifunga Lindi Wanaume 122-20. Mechi za leo ni kati ya Tabora vs Kilimanjaro (Wanaume), Morogoro vs Unguja (Wanawake), Mbeya vs Pemba (Wanawake), Unguja vs Rukwa (Wanaume).

NDONDI

Mabondia Mtuchoma Costa na Yonas Godfrey watapanda ulingoni Desemba 25 kusherehekea sikukuu ya X-Mass katika ukumbi wa Friends Corner Manzese.

TENIS

Michuano ya Tenis ya Davis kanda ya Sita kwa wachezaji wenye umri wa miaka 14-25 itakayofanyika 2012 jijini Dar es Salaam. Tayari timu ya Dar es Salaam imeweka kambi Tanga kwa msaada wa Kampuni ya Tanga Cement.

CHAMIJATA
Chama cha Michezo ya Jadi nchini (CHAMIJATA) kimetembeza bakuli. Mwenyekiti wa CHAMIJATA mzee Kazi Ngumbe amesema wanatafuta mdhamini ili kufikia malengo ya 2012, pia kuandaa uchaguzi mkuu wa chama.

No comments:

Post a Comment

Post a Comment